Job 17:1-6

1 aMoyo wangu umevunjika,
siku zangu zimefupishwa,
kaburi linaningojea.

2 bHakika wenye mizaha wamenizunguka;
macho yangu yamebaki kutazama uadui wao.

Ayubu Anaomba Msaada


3 c“Ee Mungu, nipe dhamana unayodai.
Ni nani mwingine atakayeweka dhamana kwa ajili yangu?

4 dUmezifunga akili zao zisipate ufahamu,
kwa hiyo hutawaacha wapate ushindi.

5 eKama mtu akiwashutumu rafiki zake ili apate ujira,
macho ya watoto wake yatashindwa kuona.


6 f“Mungu amenifanya kitu cha dhihaka kwa kila mtu,
mtu ambaye watu humtemea mate usoni.
Copyright information for SwhKC